Lupita Nyong’o
ameonekana kwa mara ya kwanza akiwa na mpenzi wake mpya mwanamitindo mwenye
asili ya Nigeria, Mobolaji Dawodu.
Wawili
hao wameonekna Jumanne hii kwa mara ya kwanza wakiwa pamoja kwenye mchezo wa
tennis kwenye mashindano ya US Open huko jijini New York wakati Serena Williams
alipokuwa akicheza na Ekaterina Kakarova.
Siku
chache zilizopita Lupita alithibitisha kuwa na mahusiano na mwanamitindo huyo
huku akidai kuwa amemua kumweka mahusiano yake mitandaoni baada ya kumchunguza
kwa muda wa miezi sita.
Dawodu
ni mwanamitindo lakini pia ni muhariri wa jarida la mitindo GQ la nchini
Marekani.

No comments:
Post a Comment