
Ikiwa ni siku kadhaa zimepita tangu litokee tukio la kuanguka ndege ya Egyptian Air May 19 2016, taarifa nyingine iliyoripotiwa leo May 27 2016 inahusu ndege ya Korean air aina ya Boeing 777 kupasuka injini moja ya kushoto na kuwaka moto dakika chache kabla ya kupaa katika uwanja wa ndege wa Haneda Tokyo kuelekea Seoul.

Taarifa zilizotolewa na Japan Television zinasema ndege hiyo iliyokua na abiria 307 na crew ya watu 17 walihamishwa kwa haraka kwenye ndege hiyo lakini bado moto huo uliwajeruhi watu 7 wakiwemo wanaume wawili na wanawake watano.
Mabasi mawili ya zima moto yalifika eneo la tukio na kuzima moto huo, chanzo cha itilafu ya ndege hiyo bado hakijajulikana na uchunguzi bado unaendelea.



abiria waliokuwa kwenye ndege hiyo

No comments:
Post a Comment