Putin asitisha mkataba wa nyuklia kati ya Urusi na Marekani - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday 4 October 2016

Putin asitisha mkataba wa nyuklia kati ya Urusi na Marekani

Makombora ya Topol RS-12M yakiwa nje ya Moscow, 2008
Urusi imesitisha mkataba wake na Marekani kuhusu kutupwa kwa madini ya ziada ya plutonium ambayo yanaweza kutumiwa kuunda silaha, ishara ya kudorora kwa uhusiano kati ya mataifa hayo mawili yenye ushawishi mkubwa duniani.

Kupitia agizo rasmi, Rais Vladimir Putin ameituhumu Marekani kwa kuunda "kikwazo cha kutishia utathabiti, kwa kuchukua hatua zisizo za kirafiki" dhidi ya Urusi.
Bw Putin alisema Urusi imelazimika kuchukua "hatua za dharura kulinda usalama wa taifa la muungano la Urusi".
Moscow imetoa masharti ya kutimizwa na Marekani kabla ya kurejelewa kwa mkataba huo.
Chini ya mwafaka huo wa mwaka 2000, kila taifa linapaswa kuangamiza tani 34 za madini ya plutonium kwa kuyachoma kwenye vinu vyake.
Mpango huo ni sehemu ya juhudi za kimataifa za kupunguza silaha za nyuklia.
Wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema tani 68 za madini ya plutonium ambazo zingeangamizwa "zinatosha kuunda silaha 17,000 za nyuklia".
Pande zote mbili zilikuwa zimetia saini upya mkataba huo mwaka 2010.
Kwingineko, Marekani nayo imetangaza kwamba itasitisha mazungumzo na Urusi kuhusu mzozo Syria.
Marekani imesema Urusi haijatimiza masharti yaliyoafikiwa chini ya mpango wa kusitisha mapigano kwa muda mwezi jana, ambao umesambaratika.
Urusi imesema hatua hiyo ni ya kusikitisha na badala yake ikailaumu Marekani kwa kujaribu kuiwekea lawama Urusi.
Bw Putin aliwasilisha mswada kwa bunge la taifa hilo ambao unaeleza masharti yanayofaa kutimizwa na Marekani kabla ya kurejelewa kwa mkataba huo wa madini ya plutonium.
Masharti hayo ni pamoja na:
§  Kupunguzwa kwa wanajeshi wa Marekani na silaha zake katika nchi zilizojiunga na Nato baada ya 1 Septemba 2000
§  Kuondolewa kwa vikwazo vyote vya Marekani dhidi ya Urusi na kulipwa fidia kutokana na madhara yaliyotokana na vikwazo hivyo.

Marekani pamoja na Umoja wa Ulaya waliiwekea Urusi vikwazo kufuatia hatua ya Moscow ya kuchukua jimbo la Crimea kutoka kwa Ukraine mwaka 2014, pamoja na hatua ya Urusi ya kuunga mkono wapiganaji wanaotaka kujitenga kwa maeneo ya mashariki kwa Ukraine.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here