Zuma asubiri uamuzi kuhusu mashtaka - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, 23 May 2016

Zuma asubiri uamuzi kuhusu mashtaka

Silaha
Waendesha mashtaka mkuu nchini Afrika Kusini wanatarajiwa kufichua leo iwapo watafufua mamia ya mashtaka ya ulaji rushwa dhidi ya Rais Jacob Zuma au la.
Hii ni kufuatia uamuzi wa mahakama mwezi jana ambayo ilisema uamuzi wa kutupilia mbali mashtaka hayo haukuwa wa busara na unafaa kutafakariwa upya.

Mashtaka hayo yanajumuisha kashfa kubwa ya mabilioni ya dola ya ununuzi wa silaha iliyofutiliwa mbali mwaka 2009.
Zuma
Kufutiliwa mbali kwa mashtaka hayo kulimfungulia njia Bw Zuma kushinda urais wiki chache baadaye.
Wachanganuzi wa masuala ya kisiasa wanasema iwapo mashtaka hayo yatafufuliwa, basi hatua hiyo itaongoeza shinikizo za kumtaka Bw Zuma ajiuzulu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here