Mwanamke kijana kutoka Pakistan aliyedaiwa kuchomwa hadi kufa na mamaake mzazi kwa kuolewa bila ruhusa ya familia yake amezikwa.
Zeenat Rafiq amezikwa na familia ya mumewe mjini Lahore.
Maafisa wa polisi wamesema hakuna hata nduguye mmoja aliyewasili kuchukua mwili wake.
Mamake kwa sasa anazuiliwa na polisi akituhumiwa kwa kumchukua kutoka kwa wakwe zake.
Msichana aliyechomwa hadi kufa
Ni kisa cha tatu katika kipindi cha mwezi mmoja nchini Pakistan ambapo mashambulio dhidi ya wanawake wanaokwenda kinyume na sheria za kihafidhina kuhusu mapenzi na ndoa ni mengi.
Maafisa wa polisi wanasema kuwa mwili wa Zeenat Rafiq ambaye alikuwa na umri wa miaka 18 ulionyesha ishara za mateso.
Alimwagiwa mafuta na kuchomwa.

No comments:
Post a Comment