Tuzo, nguo za red carpet na mali zingine za marehemu Whitney Houston zitapigwa mnada June 24 na 25.
Mnada huo utasimamiwa na kampuni ya Heritage Auctions na familia yake.
Jumla ya vitu 119 vilivyomilikiwa na muimbaji huyo vitauzwa. Hati yake ya kusafiria ni miongoni mwa vitu hivyo.
Pia ipo shela aliyoivaa kwenye harusi Bobby Brown mwaka 1992.
Houston alifarili February 11, 2012, kwenye hoteli huko Beverly Hills, California nchi Marekani.

No comments:
Post a Comment