Majanga mapya tena kwenye show ya Snoop Dogg na Wiz Khalifa, 11 walazwa - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, 10 August 2016

Majanga mapya tena kwenye show ya Snoop Dogg na Wiz Khalifa, 11 walazwa

     wiz-khalifa_0

Ziara ya ya Snoop Dogg na Wiz Khalifa imeendelea kukumbwa na majanga.

Jumanne hii, watu 50 wengi wao wakiwa vijana wenye umri mdogo, walilewa chakali kiasi cha kuhatarisha maisha yao (alcohol poisoning). Wasanii hao wapo kwenye ziara ya pamoja iitwayo The High Road Tour.
11 kati ya watu hao walilazwa kwenye hospitali za jirani akiwemo kijana mwenye miaka 18 ambaye alianguka chini na kuvunja pua yake. Watu kadhaa pia walishikwa kwa kukutwa na bangi kwenye show hiyo.

Vyanzo vimedai kuwa vijana hao walikuwa wakinywa vodka zilizokuwa kwenye chupa za maji kwenye vyo na sehemu ya kuegeshea magari. Tukio hilo limekuja siku chache tu baada ya watu 42 kuumia baada ya kuanguka kwa uzio kwenye show yao ya Camden, NJ.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here