KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday, 7 March 2016

KUELEKEA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

unnamed (26)

unnamed (26)

Tarehe 08 Machi kila mwaka Tanzania huungana na nchi nyinge wanachama wa 
Umoja wa Mataifa katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani.

11042216_862640687115659_420877251_n
11042216_862640687115659_420877251_nLENGO LA MAADHIBISHO HAYA 
  • Hutoa fursa kwa Serikali, wananchi, wadau, na wanawake wenyewe Kupima utekelezaji wa maazimio, matamko na mikataba  inayohusu masuala ya maendeleo ya wanawake na usawa wa jinsia!
  • Siku ya wanawake duniani husisitiza kujenga mshikamano wa wanawake wote duniani, kuhamasisha jamii kutafakari kauli mbiu husika.
  • Maadhimisho ya Siku ya Wanawake ya kila mwaka huelimisha jamii kuhusu jitihada mbalimbali zilizofanywa na Serikali na asasi kadha wa kadha katika kuwaendeleza wanawake na kuhamasisha jamii kuhusu utekelezaji wa sera na mipango mbalimbali ya Serikali yenye lengo lakudumisha Amani, Usawa na Maendeleo.
MAK32
KAULI MBIU  YA MWAKA HUU
Kauli mbiu ya mwaka 2016 ni “50-50 ifikapo 2030: tuongeze jitihada”
 KWANINI?
Kauli mbiu hii inasisitiza kuwa na mikakati thabiti yenye mwelekeo wa kufikia Agenda  ya malengo ya millenia inayohimiza kufikia asilimia 50 -50 ya ushiriki wa wanawake na wasichana katika nyanja zote za maendeleo.Kuanzia mwaka 2005 Serikali ilipitisha uamuzi kuwa maadhimisho haya yafanyike kitaifa kila baada ya miaka mitano kutoa muda wa utekelezaji wa maazimio na kupima mafanikio yaliyofikiwa katika kipindi cha miaka mitano.Mwaka 2015 Maadhimisho yalifanyika kitaifa mkoani  Morogoro. Mwaka huu  2016 mikoa yote itaadhimisha siku hii katika maeneo yao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here