Msanii wa Bongo Fleva, Malaika amesema kuwa tangu ameanza muziki hajawahi kuwa na menejimenti ila kuna watu wamejitokeza kutoka Norway wapo tayari kufanya hivyo.

Alikuwa akiongea kwenye kipindi cha Hatua Tatu, kinachoruka kupitia Times FM.
“Sikuwahi kuwa na meneja tangu naanza muziki, wapo watu ambao wananisupport. Hata wewe ukipenda unanisupport, ili kuna watu wa Norway wapo tayari kunisimamia ikiwa tayari nitawajulisha,” alisema Malaika.

No comments:
Post a Comment