Bob Junior amesema kwa sasa ana jina jipya katika unenguaji wake wa viuno jukwaani.

Akiongea na kipindi cha Twenzetu cha Times FM, msanii huyo anayemiliki studio za Sharobaro Records alisema viuno vyake vitafahamika kwa jina la ‘Viuno vya Nazi Mbata.’
“Sasa hivi viuno vyangu vinaitwa viuno vya nazi mbata, ni jina jipya, na nimemodify zaidi kukatika,” alisema muimbaji huyo.
Hivi karibuni muimbaji na producer huyo aliachia wimbo wake aliomshirikisha msanii wa Uganda, Jose Chameleone.

No comments:
Post a Comment