Mpango wa kuunda gari hilo lililopewa jina Bloodhound ulikwama
miezi ya karibuni kutokana na matatizo ya kifedha.
Lakini
mfadhili mpya amepatikana na wahandisi wanaweza sasa kkurejelea kazi ya
kulitengeneza.
Oktoba 2017 itakuwa miaka 20 tangu kuwekwa kwa rekodi ya sasa ya
kasi ya gari ardhini ambayo ni kilomita 1,228 kwa saa (763mph).
Rekodi hiyo iliwekwa na gari lililopewa jina Thrust SSC jangwani
Marekani.
Wanaounda Bloodhound wanatarajia gari hilo liweze kufikia kasi ya hadi kilomita 1,287 kwa saa nchini Afrika Kusini.
Gari hilo linaundiwa Uingereza.
Gari hilo liliwasilishwa kwa maonesho Canary Wharf, London
likiwa bado halijakamilika mwezi Septemba mwaka jana.
Tangu wakati huo, limekuwa Bristol likiwa halifanyiwi kazi
yoyote.
Gari hilo litatumia injini ya ndege aina ya Eurofighter-Typhoon
ambayo itaundwa na kampuni ya Nammo ya Norway.
Gia yake itaundwa na wahandisi wa mradi huo wa Bloodhound na
pampu yake itakuwa ya Jaguar V8.
Litafanyiwa majaribio Cornwall, Uingereza mwezi Mei au Juni
mwaka ujao.

No comments:
Post a Comment