PICHA 4 Za Gari Ya Seed zaidi Duniani Jionee - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, 8 July 2016

PICHA 4 Za Gari Ya Seed zaidi Duniani Jionee


Mradi wa kuunda gari liendalo kasi Zaidi duniani umefufuliwa na gari hilo linatarajiwa kujaribu kuvunja rekodi ya dunia mwaka ujao.


Mpango wa kuunda gari hilo lililopewa jina Bloodhound ulikwama miezi ya karibuni kutokana na matatizo ya kifedha.
Lakini mfadhili mpya amepatikana na wahandisi wanaweza sasa kkurejelea kazi ya kulitengeneza.
Oktoba 2017 itakuwa miaka 20 tangu kuwekwa kwa rekodi ya sasa ya kasi ya gari ardhini ambayo ni kilomita 1,228 kwa saa (763mph).
Rekodi hiyo iliwekwa na gari lililopewa jina Thrust SSC jangwani Marekani.

Wanaounda Bloodhound wanatarajia gari hilo liweze kufikia kasi ya hadi kilomita 1,287 kwa saa nchini Afrika Kusini.
Gari hilo linaundiwa Uingereza.
Gari hilo liliwasilishwa kwa maonesho Canary Wharf, London likiwa bado halijakamilika mwezi Septemba mwaka jana.
Tangu wakati huo, limekuwa Bristol likiwa halifanyiwi kazi yoyote.
Gari hilo litatumia injini ya ndege aina ya Eurofighter-Typhoon ambayo itaundwa na kampuni ya Nammo ya Norway.
Gia yake itaundwa na wahandisi wa mradi huo wa Bloodhound na pampu yake itakuwa ya Jaguar V8.
Litafanyiwa majaribio Cornwall, Uingereza mwezi Mei au Juni mwaka ujao.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here