Watu 19 wauawa kituo cha walemavu Japan - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Tuesday, 26 July 2016

Watu 19 wauawa kituo cha walemavu Japan

Japan
Watu 19 wameuawa nchini Japan baada ya mtu mmoja kuwashambulia watu kwa kisu katika kituo kimoja cha walemavu, kilichoko katika mji wa Sagamihara, magharibi mwa mji mkuu Tokyo. Watu zaidi ya 20 wamejeruhiwa, wengi wao vibaya.

Ripoti nchini Japan zinasema kuwa mtu mmoja ambaye alikuwa akifanya kazi katika kituo hicho cha Tsukui Yamayuri-en, alijipeleka hadi kituo cha polisi na kukiri kuwa ndiye aliyetekeleza mauaji hayo ya kutisha na kwa sasa anazuiliwa.
Mtu huo ametambuliwa kama Satoshi Uematsu, mwenye umri wa miaka 26.
Polisi wanasema mshukiwa alikuwa amemwandikia barua spika wa bunge la chini mwezi Februari akitishia kuwaua walemavu.
Alitibiwa hospitali lakini baadaye akaachiliwa.

Visa vya mauaji ya watu wengi kwa pamoja huwa nadra sana nchini Japan.
    
Visa vya watu kuchomwa visu mwaka 2001 na 2008 vilisababisha vifo vya watu saba na wanane mtawalia.
Mwaka 1995, shambulio la kutumia gesi ya sumu ya sarin katika treni mjini Tokyo, ambalo lilitekelezwa na watu wa madhehebu ya Aum Shinrikyo, lilisababisha vifo vya watu 12.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here