Chris Brown amekamatwa
na polisi wa LAPD kwa madai kuwa amemtishia mtu kwa silaha nzito.
Baylee
Curran alimshutumu Brown kwa kumtishia na bunduki yake huko Tarzana, Calif.
Mrembo huyo aliyekuwa akijirusha na Brown kabla ya hapo, anadai kuwa ugomvi
ulizuka baada ya kuonesha kutamani midani zake za madini.
Muimbaji
huyo alidai kumfukuza msichana huyo na kumtishia na bunduki.
Maofisa
wa polisi waliwasili kwenye eneo la tukio saa tisa alfajiri Jumanne hii baada
ya simu ya 911 kupigwa na mwanamke aliyehitaji msaada. Curran alipeleka mashtaka
polisi na kukatolewa hati ya kufanywa msako.
Wakati
wa uchunguzi, Brown anadaiwa kutupa begi lake dogo nje ya dirisa ambamo
kulikuwa na bunduki mbili na madawa, kwa mujibu wa mtandao wa TMZ.
Baada
ya kulitupa, Breezy anadaiwa kupiga yowe ‘come and get me.’
Kwa
sasa amechukuliwa kwenye kitengo cha ‘Robbery Homicide’ kwenye LAPD.
Awali,
Brown alitumia Instagram kukanusha madai hayo.

No comments:
Post a Comment