Rais wa zamani wa Ufaransa , Nicolas Sarkozy,
amethibitisha kuwa atawania tena kiti hicho.
Bw Sarkozy alishindwa na rais wa
sasa Francois Hollande miaka minne iliyopita.
Wakati huo alisema kuwa anastaafu
katika ulingo wa siasa, lakini katika kipindi cha miaka miwili alirejea katika
harakati za kampeni.
Bw Sarkozy ni mmoja kati ya watu
kadhaa wanaowania uteuzi wa kugombea urais kupitia chama cha mrengo wa kati na
kulia akiwemo waziri mkuu wa zamani Francois Fillon, na waziri wa mambo ya
kigeni Alain Juppe.
Bw Sarkozy anakabiliwa na kesi ya
ufisadi na kujaribu kutoa rushwa katika uteuzi wa hakimu wa mahakama kuu ili
atowe taarifa kuhusu uchunguzi kuhusiana na udhamini wa kisiasa.

No comments:
Post a Comment