Mr Blue: Mke wangu akisema ‘Yes’ hakuna wa kunibabaisha! - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, 8 September 2016

Mr Blue: Mke wangu akisema ‘Yes’ hakuna wa kunibabaisha!

  13408824_238905193159819_1442580974_n
Mr Blue amesema kwa sasa amekuwa mtu mzima na kwamba mambo ya kupiga pamba kama zamani amewaachia wasanii vijana zaidi.

Akiongea na Clouds Fm, rapper huyo amesema kama mke wake atapenda anachovaa, hakuna kinachompa mawazo tena.
“Unajua unapokuwa pia na mambo nayo yanabadilika, najitahidi sasa hivi navaa simple, lakini nimependeza siwezi tena kuvaa yale manguo sijui makubwa au unikute nimevaa kijinsi sijui kimenibana au kipo kama sketi siwezi,” alisema.

“Na wala huwa sina sijui role model, nikienda dukani hiki kizuri navaa. Mke wangu ambaye ndio nimemuoa akiniambia yeye nimependeza inatosha kabisa, hata kama nimevaa taulo natoka nalo tu mambo ya kwenda na wakati sasa nawaachia wadogo zangu kama akina Young Killer, Jux,” alisisitiza Blue.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here