
Wananchi mkoani Geita wameiomba Serikali kuanza kuwapatia Mabaki ya Mawe Maarufu Magwangala kama ilivyo elekezwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakati wa Ziara yake mkoani hapa.
Rais Magufuli alifanya Ziara yake mnamo julai 30 mwaka huu mkoani hapa na kukutana na kilio cha Wananchi wanaodai kuwekewa zuio la kutumia mawe yenye mabaki ya dhahabu (magwangala) kwa lengo la kusaga na kuchenjua ili kupata dhahabu, ndipo akatoa muda wa wiki tatu kwa Wizara ya Nishati na Madini kwa kushirikiana na baraza la taifa la hifadhi na usimamizi wa mazingira (NEMC) kufanya tathimini na kuwaruhusu Wachimbaji wadogo kutumia Magwangala.
Wakizungumza kwa Nyakati tofauti baadhi ya wananchi mkoani hapa wamesema kuwa tangu Rais Magufuli atoe kauli hiyo ni takribani mwezi mmoja umekwisha kupita lakini bado hawajaanza kupewa Magwangala hayo hali ambayo imekuwa ikiwapa wasiwasi na kushindwa kujua ni lini hatima hiyo itakamilika.
Hata hivyo mmoja kati ya Viongozi wa baadhi ya vikundi vilivyoundwa kwa ajili ya kupatiwa Magwangala ambaye yeye ni Katibu wa kikundi kimoja hapa mjini kinachofahamika kwa jina la Majiko group chenye makazi yake Mtaa wa Msalala road uliopo wilayani na mkoani hapa Bw.Elia Elinathani ambapo amesema kuwa amekuwa akilifuatilia mara kwa mara jambo hilo.
Suala hili Mkuu wa Wilaya ya Geita, Herman Kapufi ametoa ufafanuzi juu ya hayo madai wakati alipokuwa katika moja kati ya ziara zake za kikazi katika kata ya Bujura mkoani Hapa.
No comments:
Post a Comment