Waziri Mkuu kuhamia Dodoma baada ya vikao vya Bunge kuisha - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday, 1 September 2016

Waziri Mkuu kuhamia Dodoma baada ya vikao vya Bunge kuisha

                   pic+pm

Serikali ya mkoa wa Dodoma imeahirisha mapokezi ya Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa yaliyokuwa yafanyike leo hadi hapo vikao vya Bunge vinavyoanza Jumanne wiki ijayo vitakapomalizika.

Akizungumza jana Mkuu wa Mkoa huo, Jordan Rugimbana alisema mkoa unajipanga namna ya kumpokea Waziri mkuu baada ya vikao hivyo kumalizika na hivyo.
Aidha Rugimbana alisema ujio wa Waziri Mkuu mjini humo bado uko palepale na kwamba maandalizi ya namna ya kumpokea yanaendelea.
Kamati za Bunge 12 zimekuwa zikiendelea na vikao vyake mjini Dodoma kwa wiki ya pili mfululizo. Wiki iliyopita Mkuu wa Wilaya ya Dodoma Mjini, Christina Mndeme, alisema Waziri Mkuu angepokelewa katika eneo la Mtumba, kisha kuzungumza na wakazi wa Dodoma katika Uwanja wa Jamhuri.
Uamuzi wa kuhamia rasmi Septemba Mosi ulitangazwa na Waziri Mkuu mwenyewe katika maadhimisho ya siku ya mashujaa Julai 25 mwaka huu yaliyofanyika mjini hapa.
CHANZO: MWANANCHI

BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here