Kimbunga hicho kimesababisha tufani ambayo imefikia kiwango cha
daraja la tatu.
Kimbunga hicho kina upepo unaosafiri kwa kasi ya zaidi ya
kilomita 200 kwa saa.
Inakadiriwa kwamba kimbunga Nicole kitafikia eneo hilo ambalo
linamilikiwa na Uingereza baadaye Alhamisi.
Maafisa wa serikali wamewahimiza watu kusalia manyumbani.
Wiki iliyopita, kimbunga kingine kwa jina Matthew kilipiga
maeneo ya Haiti na kuua mamia ya watu.
Mafuriko yaliyotokana na kimbunga Matthew pia yalisababisha
uharibifu Jamaica, Jamhuri ya Dominika, Jamaica na majimbo ya Florida na
Carolina Kaskazini nchini Marekani.

No comments:
Post a Comment