Kituo cha sheria na haki za binadamu LHRC kimeiomba serikali kuondoa
adhabu ya kifo kutokana na adhabu hiyo kuenda kinyume na haki za binadamu na
kuathiri kiasi kikubwa haki za msingi ya kuishi.
Akitao
tamko juu ya siku ya maadhimisho ya kupinga adhabu ya kifo duniani ,mkurugenzi
mtendaji wa kituo hicho Dk Hellen Kijo Bisimba amesema adhabu ya kifo imekuwa
kinyume na siyo sahihi.
“Adhabu hii inakuwa kama ya
kulipiza kisasi,kwasababu haimsaidii yule aliyekufa zaidi ya kuongeza mtu
mwingine kufa, hata ndugu wanaosema ndugu yetu amekufa akiuawa huyo aliyeuwa
wao hawampati tena ndugu yao kwahiyo haisaidii,” alisema.
“Lakini pia utafiti haujaweza
kutuonyesha kwamba adhabu hii imesaidia kuondoa hilo tatizo,” aliongeza
Bisimba.
Tanzania ni miongoni mwa nchi
ambazo zimekuwa zikishinikizwa na mashirika ya kimataifa hasa yale ya utetezi
wa haki za binadamu kufuta sheria hiyo.
Machi 6 mwaka huu Kamishna wa haki
za binadamu katika Umoja wa Mataifa, Navi Pillay alinukuliwa kupitia Idhaa ya
Kiswahili ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC) akilaani kuendelea kwa
adhabu hiyo alioyoiita kuwa ni ‘ukatili dhidi ya binadamu.’
Zaidi ya watu 360 wanasubiri adhabu
hiyo nchini.
BY: EMMY MWAIPOPO
No comments:
Post a Comment