Msichana mmoja chini ya miaka 15, huolewa kila baada ya sekunde 7, kwa
mujibu wa ripoti mpya ya shirika la Save the Children.
Utafiti
huo umesema kuwa wasichana wenye miaka 10 wanalazimishwa kuolewa na wanaume
wenye umri mkubwa katika nchi zikiwemo Afghanistan, Yemen, India na Somalia.
Migogoro, umaskini na matatizo ya
kibinadamu, yameonekana kuwa ni chanzo cha kuwaacha wasichana wakiwa hatarini
kuolewa wakiwa na umri mdogo.
“Wasichana wanaolewa wakiwa na umri
mdogo hawawezi kwenda shule, wana hatari ya kukabiliana na unyanyasaji wa majumbani,
kufanyiwa ukatili na kubakwa. Hupata mimba na wanakuwa hatarini kupata magonjwa
ya zinaa ikiwemo HIV,” amesema ofisa mtendaji mkuu wa Save the Children
International Helle Thorning-Schmidt.
Ripoti hiyo imepewa jina, Every
Last Girl na imekuangikia kwenye siku ya kimataifa ya msichana, Jumanne hii.
No comments:
Post a Comment