Mke wa rais wa Marekani, Michelle Obama, anatarajia kufanya
mahojiano ya moja kwa moja na wasichana 25 wa kitanzania lengo likiwa ni
kumwezesha msichana katika masuala mbalimbali ya upatikanaji wa fursa.
Majadiliano hayo yatafanywa na Shirika la Plan
International Tanzania na yatafanyikia katika ubalozi wa Marekani, wakati wa
maadhimisho ya siku ya msichana duniani, Jumanne hii Oktoba 11, 2016.
Mkurugenzi mkazi wa Plan
International, Jorgen Haldoresn, alisema katika kuadhimisha siku hiyo wadau
wataombwa kuunga mkono jitihada zinazofanywa na kundi hilo na kupewa nafasi ya
kujifunza, kuongoza, kuamua na kuishi ili kuonesha thamani ya mtoto wa kike na
hata kwa kuwapa fursa sawa.
Mkurugenzi huyo amesema nchi
nyingine zitakazoshiriki katika majadiliano na mke wa Obama ni Peru na
Cambodia.
BY: EMMY MWAIPOPO
No comments:
Post a Comment