Polisi kanda maalumu ya Dar es Salaam, imefanya operesheni katika maeneo
ya katikati na pembezoni mwa jiji la Dar es Salaam na kuwakamata watuhumiwa 87
wa makosa mbalimbali, wakiwemo waliokuwa kwenye mtandao wa uhalifu wa mkazi wa
Machimbo Yombo jijini Dar es Salaam, Salim Njwete (34) maarufu kama ‘Scorpion’.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Jumatatu hii, Kamanda Sirro amesema
watuhumiwa wengine wanadaiwa kuvunja nyumba na kuiba na wengine walipatikana na
gongo lita 148, bangi kete 95 na puli 48.
“Watuhumiwa hao walipatikana na
makosa mbalimbali yakiwemo kuvunja nyumba usiku na kuiba ndani kuvuta, na kuuza
bangi, kuuza na kunywa gongo, kupiga debe, uzembe na uzururaji,” alisema
Kamanda Sirro.
Njwete (Scorpion) alifikishwa
katika Mahakama ya Wilaya ya Ilala mwishoni mwa wiki, kujibu mashitaka ya
unyang’anyi wa kutumia silaha na kumtoboa macho yote mawili Said Ally Mrisho.
Aidha kamanda Sirro alisema
watuhumiwa hao, wamekamatwa kwa nyakati tofauti katika maeneo ya Mbagala,
Buguruni, Kiluvya, Gongo la Mboto, Tandika, Ukonga, Banana, Kunduchi, Keko,
Kawe.
BY: EMMY MWAIPOPO
No comments:
Post a Comment