Mwaka 1994 alikuwa na umri wa miaka 17 akiishi nchini
Rwanda kwenye familia moja tajiri na ndoto yake ilikuwa ni ya kuwa muimbaji
maarufu.
Lakini maisha ya Corneille Nyungura
yalichukua mkondo mwingine kwa ghafla wakati yalitokea mauaji ya kimbari ya
mwaka mwaka 1994 wakati takriban watu 800,000 wa kabila la watusi na wahutu
wachache wenye msimamo wa wastani waliuawa.
Wakati kundi la wauaji lilipowasili
nyumbani kwao, Corneille alijificha nyuma ya sofa wakati familia yake yote
ilichinjwa
Sasa yeye ni raia wa Canada na mmoja wa wanamuziki bora
zaidi wa RnB kutoka nchini Rwanda na amekuwa akiimba kwa miaka 20 iliyopita
Akijaribu kukubaliana kile
kilichotokea nchini mwake mwaka 1994, Corneille anasema kuwa na uoga wa kurudi
nyumbani kwao.
No comments:
Post a Comment