Vyombo vya habari vya Reuters na
kile cha Yonhap kutoka Korea kusini vimewanukuu baadhi ya maafisa ambao
hawakutajwa majina wakisema kuwa kampuni hiyo imesitisha kwa muda utengezaji wa
simu hizo.
Samsung imeambia BBC inaimarisha
utengezaji wa simu hizo ili kuhakikisha ubora na usalama wake.
Hatua hiyo inajiri baada ya kampuni
mbili nchini Marekani kusitisha uuzaji wa simu hizo .
Samsung ilisema siku ya Jumatatu
pia itazuia usafirishaji wa simu hizo katika maeneo tofauti duniani ili
kuzifanyia ukaguzi.
Kampuni hiyo ya Korea Kusini
ilizirudisha simu hizo mnamo mwezi Septemba na kuwahakikishia wateja wake mwezi
uliopita kwamba simu zilizorekebishwa ziko salama.
Lakini kumekuwa na ripoti nyengine
tofauti za simu zilizorekebishwa kutoa moshi.
No comments:
Post a Comment