Rais Magufuli Alivyoshiriki Ibada na kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa Chato - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Monday 17 July 2017

Rais Magufuli Alivyoshiriki Ibada na kuendesha harambee ya ujenzi wa Kanisa Chato

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr John Magufuli jana alisali Ibada ya Jumapili ya 15 ya mwaka wa Kanisa iliyofanyika katika Kanisa la Bikira Maria Parokia ya Chato Mkoani Geita na kuendesha harambee ya kuchangia ujenzi wa kanisa hilo.

Katika harambee hiyo Mhe. Rais Magufuli ambaye aliongozana na Mkewe Mama Janeth Magufuli alifanikiwa kuchangisha fedha taslimu kiasi cha Shilingi Milioni 13, ahadi Shilingi 920,000/=, mifuko ya saruji 33 na malori 2 ya mchanga.

Mhe. Rais Magufuli aliwapongeza waumini wa Parokia ya Chato kwa hatua kubwa waliyopiga katika ujenzi wa kanisa kuu la Parokia hiyo na amewataka kuendelea kujitolea kukamilisha hatua za mwisho za ujenzi huo.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here