Madee amewakumbusha
Dogo Janja na Raymond wasisahau walipotoka.
Kupitia
akaunti yake ya Instagram, Madee ameandika:
HUSIA
KWA WANANGU/c mnakumbuka kule tumetoka eeh…si mnakumbuka tulivokua tunakula
eeh..c mnakumbuka tulivokua tunalala een…c mnakumbuka tulivokua tunachekwa
eeh..sasa hawatucheki wanatushangilia. .msidanganywe na mliowakuta mjini..haswa
marafiki wakike fake na wakiume fake..nafasi zenu zinagombaniwa na watu
wengi..mkizubaa tu wamezichukua..fanyeni maisha kwanza!!! Mimi najivunia nyinyi
@dogojanjatz@rayvanny #vyutivimekaa
Wawili hao wamekuwa ni kama watoto wa Madee kwa sababu ndiye
aliyewasaidia kuushawishi uongozi wa kundi la Tip Top kuwapokea kwa mara ya
kwanza.

No comments:
Post a Comment