Baada ya ushindi
kinachofuata ni kusherehekea. Na hakuna sherehe nzuri kama unapomchukua mama
yako mzazi na mwanao kuwapeleka kwenye kisiwa cha raha duniani, Ibiza, Hispania.
Mchezaji huyo wa Real
Madrid na Ureno iliyoshinda kombe la Ulaya majuzi ameenda kisiwani humo kwa
mapumziko anayoyatumia kula bata kwenye yacht
Jumatano hii
ameonekana akichomwa jua la Ibiza ndani ya yacht ya kifahari akiwa na mama yake
Delores na mwanae, Cristiano Jr. Kuonesha kuwa tamaduni zetu na zao ni tofauti,
Ronaldo ameonekana kwenye picha hizo za mapaparazi akiwa na kipensi kifupi huku
mama yake akiwa ndani ya bikini tu.
. Kwenye picha
nyingine Ronaldo anaonekana akifanyiwa massage na mama yake.

No comments:
Post a Comment