
Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU),
itaanza kudahili wanafunzi waliomaliza kidato cha sita wanaoomba kujiunga na
vyuo vikuu kuanzia kesho.
Akizungumza jana, Kaimu Mkurugenzi
wa Udahili na Nyaraka wa TCU, Dk Kokubelwa Mollel alisema udahili kwa wenye
diploma utaanza Julai 31.
Dk Mollel alisema kazi hiyo
itaendelea kwa mwezi mzima ili kuruhusu wananchi wengi zaidi kupata fursa ya
kuomba kudahiliwa na udahili huo utafanyika kwa njia ya mtandao.
Alisema ili wanafunzi waweze
kuelewa programu zinazotolewa na vyuo vikuu, tume hiyo imeandaa maonyesho ya 11
yatakayofanyika kuanzia Julai 20 hadi 22, mwaka huu.
Alisema maonyesho hayo yatafanyika katika
viwanja vya Karimjee jijini Dar es Salaam na kufunguliwa na Waziri wa Elimu,
Sayansi, Teknolojia na Mafunzo ya Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako.

No comments:
Post a Comment