Baada ya taarifa kuenea kwenye mitandao ya kijamii kuwa Rais
John Pombe Magufuli amemteua Jerry Murro ambaye alikuwa afisa habari wa Yanga
kuwa msaidizi wa mawasiliano ya Rais Ikulu, kurugenzi ya mawasiliano imekanusha
habari hizo na kusema kuwa sio za kweli.
Barua iliyoandikwa kutoka Ikulu imesema ‘kuna taarifa
zimesambazwa zikisema kuwa Rais Magufuli amemthibitisha Gerson Msigwa kuwa
mkurugenzi wa mawasiliano Ikulu huku msaidizi wake akiwa ni aliyekuwa msemaji
wa klabu ya Yanga Jerry Murro, taarifa hizo sio za kweli na wananchi wazipuuze'


No comments:
Post a Comment