Mkurugenzi Mkuu wa mamlaka ya ustawishaji Makao Makuu (CDA), Pascas
Mulagiri amesema kumekuwepo na ongezeko la maombi ya wizara na idara mbalimbali
za kupata viwanja ili kujenga ofisi zao Dodoma.
Amedai kuwa kufuatia agizo la Rais Dkt John Pombe
Magufuli kuhusu serikali kuhamia Dodoma, wizara, watumishi wa umma na taasisi
za serikali zimewasilisha maombi ya kugawiwa viwanja kwaajili ya ujenzi wa
majengo ya ofisi zao.
Alisema watapima ardhi ya kutosha ili kuziwezesha
wizara, taasisi, watumishi na watu watakaohamia mjini hapo kupata viwanja.
Pia aliongeza kuwa ofisi yake ina mpango wa mpito wa
kupata makazi na kuhamasisha watu wenye nyumba mjini hapo na kuzipangisha kwa
watumishi wa umma watakaohamia Dodoma .
Mulagiri alisema wameunda kamati maalum inayoratibiwa na
mkuu wa mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana ili kukamilisha azma hiyo.
BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:
Post a Comment