Msanii mkongwe wa muziki wa bongofleva, Dully Sykes baada ya kufanya
vizuri na wimbo wake mpya ‘Inde’ amesema kilichobaki kwenye muziki wake ni
kufungua milango ya kwenda kimataifa.
Akiongea na Bongo5 Jumanne hii, Dullly amesema kufanya
vizuri nyumbani kutamsaidia kutoboa zaidi kimataifa kwa kuwa mashabiki wa
nyumbani ndio wenye nguvu ya kumpush kwenda kimataifa zaidi.
“Kwa sasa plan yangu ni kwenda kifataifa, tayari
nimeshafanya kila kitu kwenye huu muziki,” alisema Dully Sykes “Ninamashabiki
ambao kwa sasa ni wazee na wengine wameshakufa na bado naendelea kutengeneza
wapya, kwa hiyo kwangu mimi vingi nimeshafanya hapa nyumbani, sasa nataka
kwenda mbele zaidi,”
Aliongeza, “Unajua katika muziki mtaji wa kwenda
kimataifa unaanzia nyumbani, lazima uwe na mashabiki wa kutosha ambao wataweza
kusupport muziki wako, kama nyumbani huna mashabiki nani atakusupport
kimataifa, kwa hiyo mimi kwangu naweza kusema safari imeiva,”
Video yake ya wimbo ‘Inde’ aliyomshirikisha Harmonize
tayari imeshaanza kuchezwa katika vituo mbalimbali vya runinga vya kimataifa
huku katika channel ya Youtube ikiwa na views zaidi na laki nane ndani ya wiki
moja.

No comments:
Post a Comment