
Majambazi ambao idadi yao haijajulikana wanadaiwa kuuwawa katika
mapigano hayo kati yao na polisi huko Vikindu, wilaya ya Mkuranga leo.
Milio ya risasi na mabomu vilisikika kuanzia saa saba usiku
katika eneo hilo ambalo majambazi hayo walikuwa wamejificha.
Habari zilizotufikia hivi punde, zinaeleza kuwa Polisi wameweka
kizuizi cha barabara eneo la Kongowe, wilayani Mkuranga ambapo magari
yote yanayotoka na kuingia Dar yanapekuliwa.

No comments:
Post a Comment