Hatimaye Diamond ameamua kusikiliza kilio cha wengi kwa si tu kuanzisha
bendi yake, bali pia kujiandaa kwa ziara ya Afrika.
Muimbaji huyo amepost video kadhaa zinazomuonesha akiwa
mazoezini na bendi hiyo na kueleza kuwa ni maandalizi ya ziara yake ya Afrika.
Miongoni mwa watu wanaonekana kwenye bendi hiyo ni
producer, Tudd Thomas.
Ziara hiyo inakuja katika kipindi ambacho staa huyo
anajiandaa kuachia album yake ya kwanza ya kimataifa.
Pia ndio itakuwa ziara yake ya kwanza ya uhakika
kuzunguka bara hilo. Bado hajesema itaanza lini na wapi.
Kwa muda mrefu mashabiki wake wamekuwa wakimshauri aanze
kutumbuiza na live band hasa kwenye show zake za kimataifa.

No comments:
Post a Comment