Msanii wa muziki wa label ya WCB, Harmonize amefunguka kwa kusema kuwa
kidogo anachokipata katika muziki wake lazima ahakikishe anakula na baby wake
ili kulinda status yake.
Muimbaji huyo ambaye anatoka kimapenzi na staa wa
filamu, Jacqueline Wolper, amesema gharaza za kumtumza mrembo huyo hazimsumbui
kama watu wanavyofikiria.
“Swala la kinywaji vyumbani kwake ana kaunta,so
akijisikia kunywa anakunywa nyumbani, mimi nirudi studio namkuta anakunywa, na
hajawai kuniambia sijui anatoka na mashoga zake,” Harmonize alikiambia kipindi
cha Enewz cha EATV.
Aliongeza, “Mwanamke yupo kwa ajili ya mwanaume
anayempenda,so kidogo nachokipata lazima nihakikishe namlinda baby wangu,
nalinda status yake.
Kwa sababu usipo muhudumia mwanamke wako, atamuhudumia
nani? atamuhudumia mtu mwingine, so kidogo nachokipata nakitunza kuhakikisha
baby wangu anapendeza vizuri na anakula anachokitaka.
Lakini sidhani kama kuna
mwanaume mjinga ambaye anaweza kutelekeza familia yake kwa ajili ya mwanamke,
kwa sababu sidhani bila Mama yangu kunizaa na kunituza ningemjua mwanamke, so
kwanza Mama yangu alafu inakuja familia yangu, na kwa sababu mwanamke wangu ni
sehemu ya familia yangu,”

No comments:
Post a Comment