Manny Pacquiao kurudi ulingoni tarehe 5 Novemba kukabiliana na Jessie Vargas - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, 5 August 2016

Manny Pacquiao kurudi ulingoni tarehe 5 Novemba kukabiliana na Jessie Vargas

        
Mwanandondi Manny Pacquiao anatarajia kulejea ulingoni mnamo tarehe 5 Novemba kukabiliana na bingwa wa dunia wa uzani wa welter Jessie Vargas kutoka Marekani.

Pacquiao, 37, bingwa wa zamani wa dunia, ametangaza kwamba atarejea licha yake kutangaza kwamba angestaafu baada ya kumshinda Timothy Bradley mwezi Aprili.
Promota wake Bob Arum alisema mwezi uliopita kwamba mwanabondia huyo kutoka Ufilipino angepigana tena mwaka huu.
“Maisha ya kustaafu hayamfai Manny kwa sasa,” meneja wa Pacquiao Michael Koncz aliambia gazeti la Los Angeles Times.
“Ndondi zimo kwenye damu yake.”
Pacquiao na kundi lake watakutana 10 Agosti mjini Manila kuamua iwapo pambano hilo dhidi ya Vargas, 27, litaandaliwa Los Angeles au Dubai.

Vargas alitwaa ubingwa mwezi Machi baada ya kushinda raia mwenzake Sadam Ali.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here