Msanii wa muziki,
Mirror hivi karibuni amepata ajali mbaya ya gari akiwa anaendesha kutoka katika
studio za AM Records pande za Tandale akielekea Ununio.
Katika
ajali hiyo, muimbaji huyo amevunjika mguu wa kulia na itachukua miezi mitatu
kukaa sawa.
“Mguu
umevunjika kabisa, kwa hiyo nimefanyiwa upasuaji na wameunga kabisa mfupa. Nipo
hospitali ya private ipo Tegeta, wamenifanyia upasuaji wakawaida, na
wameniwekea antena za ndani kwa ndani,” Mirror alikiambia kipindi cha XXL cha
Clouds FM.
Mpaka
jana muimbaji huyo alikuwa bado hajaruhusiwa kuondoka katika hospitali ambayo
amelazwa kwa ajili ya matibabu.

No comments:
Post a Comment