Q Chief hamwezi Jokate Mwegelo. Ni kwasababu anadai imeshindikana
kumtumia kwenye video yake kutokana na kile muimbaji huyo amedai mrembo huyo
alitaka alipwe ‘six figures.’
Chief ambaye jina lake halisi Abubakar Katwila amedai
kuwa amemtaja Jojo kwenye wimbo huo na kwamba ingemake sense kama angeonekana
pia kwenye chupa lakini akawa ‘very expensive.’
Akiongea na E-News ya EATV Jumatatu hii, Chief alisema
kuwa Jokate ni classmate wake hivyo alitarajia angemlegezea bei lakini Jojo
only means business.
Pamoja na hivyo, muimbaji huyo anayejiita ‘Mungu wa
Bongo Flava’ amedai kuwa anaheshimu uamuzi wa Jokate na ameongeza kuwa hawezi
kuuondoa ukweli kuwa ni mtoto mkali.
Hivi karibuni Q alishoot video mpya na Justin Campos na
kudai kuwa itawashangaza wengi.

No comments:
Post a Comment