Rais Magufuli awajulia hali Ndungai na Malecela - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, 17 August 2016

Rais Magufuli awajulia hali Ndungai na Malecela

 Rais Dkt John Magufuli, amewatembelea na kuwajulia hali spika wa bunge Job Ndugai, na Mzee John Malecela na kuwaombea dua ili waweze kurejea katika shughuli zao za kila siku.
14022162_1197381990325793_5379572732719280238_n
Rais Magufuli ambaye aliongozana na mkewe Mama Janeth, pia kumtembelea na kumjulia hali Spika wa Bunge, Job Ndugai aliyerejea hivi karibuni akitokea India alikokwenda kuangalia afya yake.


MAGUP

Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bi Janeth akifanya maombi ya pamoja
“Kiukweli nimefarijika sana nimshukuru mheshimiwa Rais kwa kuja kunitembelea na Mungu ambariki, hata kipindi nikiwa hapa nchini alikuwa akinijulia hali hata pia nilivyokuwa nimesafiri kwenda India amekuwa akinipigia simu mara kwa mara na nashukuru amekuja kwa niaba ya Watanzania, na pia niwahakikishie Watanzania kuwa naendelea vizuri, tuzidi kuombeana”,alisema Ndungai.
Naye John Malecela alisema “namshukuru Rais Magufuli pamoja na madaktari wanaonipatia matibabu, na pia hali yangu kwa sasa ni nzuri.”.
“Nawaombea kwa mwenyezi Mungu wapone na kupata nguvu haraka ili waweze kuendelea na majukumu yao kawaida ya ujenzi wa taifa,” alisema Rais Magufuli.

BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here