TFF kununua madawati fedha zitakazopatikana kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, 17 August 2016

TFF kununua madawati fedha zitakazopatikana kwenye mchezo wa Ngao ya Jamii

  TFF
Shirikisho la soka nchini (TFF) limetangaza kuwa fedha zitakazopatikana kwenye mechi ya Ngao ya Jamii zitatumika kuchangia kwenye ununuzi wa madawati kwa shule ambazo zina uhaba huo.

Mchezo huo unaotarajiwa kufanyika leo kwa kuzikutanisha timu mbili za jiji moja kati ya Yanga dhidi ya Azam FC kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam ikiwa ni ishara ya ligi kuu Tanzania Bara kuanza hivi karibuni.
Afisa habari wa TFF, Alfred Lucas amesema, “TFF haijalenga kupata mapato ya kesho “kwenye Ngao ya Jamii kwaajili ya mpango wowote wa maendeleo ya shirikisho.”

“Tumelenga kuisaidia na kuipa support serikali katika mpango wake wa kusambaza madawati kwa shule za msingi ili wanafunzi wasikae tena chini. Kwa upande wetu TFF tunatoa madawati 200,” ameongeza.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here