Label ya WCB Wasafi ya
Diamond Platnumz inafungua ofisi mpya Kijitonyama jijini Dar es salaam ambayo
itakuwa inajihusisha na masuala ya kiuongozi zaidi.
Akiongea
katika kipindi cha Clouds E cha Clouds TV Jumatatu hii, mmoja kati ya viongozi
wa juu wa label hiyo, Sallam, amesema wanafungua ofisi mpya ili kuipa nafasi
ofisi ya zamani ya kufanya shughuli zake bila kuingiliana na shughuli zingine.
“Tunafungua
ofisi nyingine ya WCB Kijitonyama,” alisema Sallam.“Hii itakuwa kwa ajili ya
viongozi, halafu ile nyingine nitaendelea na kazi nyingine,”
WCB
kwa sasa ni moja kati ya label za muziki ambazo zinafanya vizuri kutokana na
wasanii wake wengi kufanya vizuri.

No comments:
Post a Comment