Fulsa za kuchangamkia watanzania katika uwekezaji wa mafuta na gesi - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday, 2 September 2016

Fulsa za kuchangamkia watanzania katika uwekezaji wa mafuta na gesi

   picha saba
Mwenyekiti wa chemba ya biashara ya wanawake Jackline Maleko, amesema watanzania wanashabikia uwekezaji wa mafuta na gesi kwa maneno badala ya kuangalia fursa zilizopo kuanzisha miradi na kujipatia kipato.

Ameyasema hayo wakati wa kongamano la nne la watoa huduma wa sekta ya gesi na mafuta.  
Amesema ziko fursa nyingi hususan za kutoa huduma za vya chakula, ujenzi, usafirishaji, nyumba za kulala wageni na mafunzo ambavyo wawekezaji hutumia mawakala wa kutoka nje.
“Ninapenda kuwaasa watanzania hii fursa ya kuwa na gesi na oil, tunaishabikia kama vile mpira badala ya kuwa wachezaji tunakuwa washabiki. Hili la kuwa washabiki tutashtukia wenzetu wanafaidi kuliko sisi, mnavyofahamu sasa hivi soko la Afrika mashariki lina allow free movement of goods and services, sasa kama linaruhusu namna hiyo halafu sisi ni watazamaji hatushiriki,”alisema Maleko.
“Tukiangalia fursa mbalimbali zinazotokana na oil and gesi tutabaki kuandamana  tutabaki kulalamika, wakati ambapo serikali imefanya juhudi za makusudi, kuwa hata na sera ya public private partnership kuwezesha sekta binafsi kwa kushirikiana na serikali kuchukua fursa kama hii,”aliongeza.

BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here