Izzo Bizness na Abela
Music wanaounda kundi la The Amazing, Jumatano hii waliingia studio kurekodi
wimbo pamoja na msanii wa Nigeria, Ycee.
Watatu
hao waliingia studio Jumatano hii jijini Dar es Salaam. Ycee alikuwa Dar kwa
siku tatu kwaajili ya media tour na kukutana na wasanii wa Tanzania.
“Done!!!thanks
a lot hommie @iam_ycee its been a pleasure working with you #TheAmazing
#ontothenextone,” ameandika Izzo kwenye picha akiwa na staa huyo wa Omo Alhaji.
Project hiyo
imesimamiwa na producer Duppy. Ycee ameondoka leo kwenda Afrika Kusini.

No comments:
Post a Comment