Rais Magufuli awafuta machozi waliopoteza nyumba Magomeni Kota - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, 7 September 2016

Rais Magufuli awafuta machozi waliopoteza nyumba Magomeni Kota

  Image result for picha magufuli
Rais Dkt John Magufuli, amewaomba radhi wananchi 644 waliokuwa wakiishi Kota za Magomeni jijini Dar es Salaam, na kuwaahidi atakamilisha ujenzi wa nyumba zao katika kipindi cha mwaka mmoja.

Pia aliwaahidi wananchi hao kuwa watakuwa wakiishi bure kwa miaka mitano kabla ya kuuziwa nyumba hizo kwa bei ya chini kwa kufidia mateso waliyoyapata kwa zaidi ya miaka minne baada ya kuondolewa katika eneo hilo.
Akizungumza na wananchi hao, Rais alisema serikali ilichukua eneo lenye hekali 33 na ujenzi wa nyumba hizo utakaoanza katika muda wa miezi miwili kuanzia sasa na utakapokamilika kipaumbele kitapewa kwa wakazi waliokuwa wakiishi katika eneo hilo.
Kwa upande wake waziri wa ardhi, nyumba, maendeleo na makazi, William Lukuvi, alisema serikali tayari imezichukua nyumba zaidi ya 5000 katika mikoa ishirini zinazomilikiwa na shirika la nyumba la taifa ili kuepuka uwezekano wa kutapeliwa kama ilivyofanyika katika nyumba za Magomeni Kota.
Baadhi ya wananchi waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo , wameipongeza serikali kwa jitihada zake za kuwatetea wanyonge na kwamba uamuzi huo wa Rais ni habari njema kwao.
Katika hatua nyingine, Rais Magufuli ametoa siku 7 kwa taasisi zilizopanga kwenye nyumba za NHC kulipa madeni yao.
“Nimetoa siku 7 kwa taasisi zote za serikali zinazodaiwa na shirika la nyumba la taifa kulipa madeni hayo kwa mkurugenzi mkuu wa shirika hilo, uziondee taasisi zote za serikali ndani ya majengo yake kama zitashindwa kulipa katika kipindi cha juma moja,” aliagiza.

BY: EMMY MWAIPOPO

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here