Familia yagoma kuchukua
mwili wa marehemu wa mzazi wao (maiti) kwa kile kinachodaiwa
wauguzi wa hospitali teule ya rufaa ya mkoa wa Geita kuwa na majibu
machafu kwa wagonjwa.
Akizungumza na mtandao wa
madukaonline katika mazingira ya hospitali hiyo mmoja kati ya wanafamilia
ambae amefiwa na baba yake mzazi,Bahati Chihula mkazi
wa kijiji cha Kishinda kata ya Kamhanga wilayani Geita.
Amesema kuwa walimpeleka Baba yao
siku ya jumatano ya tarehe 5 mwezi huu kwa lengo la kupatiwa matibabu ya tenzi
dume lakini jambo la kusikitisha alikutana na huduma
zisizostahili za wauguzi hali ambayo imepelekea
mzazi wake kupoteza maisha kutokana na kukosa huduma nzuri za afya.
“Tulifukuzwa katika hodi ya wagonjwa kwa
madai kuwa hatutakiwi kukaa katoioka hodi hiyo na tulipotoka nje baada ya
dakika chache niliporudi nilim kuta mgonjwa wangu yupo chooni na nilipouliza
kwanini mgo njwa wangu yupo choo ni akiwa nagaragara mhuguzi alionijibu wewe
utakiwi kujua nenda zako na kutokana na huduma mbovu za hospitari hii
imepelekea kuondoa uhai wa baba yangu kwani hakuwa maututi sana na sisi kama
family hatutachukua maiti paka sheria ifate mkondo wake”Alisema Bahati.
Hata hivyo moja kati ya wananchi
ambae ana mgonjwa anaye muuguza katika hospitali hiyo Felix
Joseph ameeleza tatizo kubwa ni walinzi pamoja na wauguzi kwani
wamekuwa wakiwatusi wagonjwa na wananchi wanaokuwa wakifika katika
hosptali hiyo.
Kutokana na uzito wa swala hilo mbunge
wa Geita vijijini Joseph Msukuma amefikisha malalamiko hayo katika kikao
cha sita cha kamati ya ushauri ya mkoa kutaka kujua
utawala bora ukoje katika hospitali hiyo na juu ya hatua
zilizochukuliwa na mganga mkuu wa mkoa dhidi ya mgonjwa aliyefia chooni .
“Mwenyekiti nilikuwa nataka kuuliza
kuhusiana na utawala bora kwenye hopstari ya Mkoa Jana mpiga kula wangu
alimleta baba yake mzazi hospitarini hapo cha kusikitisha ni kwamba alifukuzwa
na kutolewa nje je ni haki naomba mganga mkuu hatujibu ameshachukua maamuzi
gani juu ya wale ambao wameshiriki katika kitendo hicho cha
unyanyasaji”aliuliza Msukuma.
Akijibu kuhusiana na tuhuma hizo za
kumwacha mgonjwa na mwisho wa siku akapoteza uhai wake mganga mkuu wa
mkoa Joseph Kasala,amefafanua kuwa walipewa mgonjwa huyo akiwa anasumbuliwa
na tenzi dume na kwamba wakati daktari ambae alitakiwa
kumfanyia upasuaji alishindwa kutokana na maumivu aliyokuwa
nayo.
Sanjari na hayo mkuu wa mkoa wa
Geita Meja Jenerali Mstafu Ezekiel Kyunga amemwagiza mganga
mkuu kwenda hospitalini hapo na kupata habari za kina na kujua ni
nani ambae amefanya uzembe wa namna hiyo na kama mtu
akibainika hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi
yake.

No comments:
Post a Comment