Wananchi wa Ludete mkoani geita wapata msaada wa mabati kwa ajili ya shule - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Wednesday, 12 October 2016

Wananchi wa Ludete mkoani geita wapata msaada wa mabati kwa ajili ya shule

Mkuu wa wilaya ya Geita Herman Kapufi  akikabidhiwa Mabati bando 20 na Mkurugenzi wa kampuni ya MUYA INVESTMENT Jua Kali Mkono kwenye ujenzi wa shule ya msingi Bwawani.


WANANCHI wa kitongoji cha njia panda kata ya Ludete wilaya na mkoa wa Geita wamesema kuwa kujengwa kwa shule ya msingi Bwawani kutasaidia kupunguza ajali za barabarani  kwa wanafunzi  ambao walikuwa wakitembea umbali wa mrefu kufuata elimu.


 Hayo  wameyasema wakati wa kupokea  msaada wa mabati bando 20 zenye thamani ya sh.milioni 5.8   yaliyotolewa na  kampuni ya( WUZHOU INVESTMENT COMPANY LTD) ambao  wanaojihusisha na uuzaji wa pikipiki aina ya San LG pamoja na vipuri .

Wananchi  wamesema kuwa  kujengwa kwa shule  hiyo kwenye kata yao pamoja na kampuni hiyo kuchangia mabati kutasaidia watoto kuacha kutembea umbali mrefu hali iliyokuwa inasababisha vifo wakati wa kuvuka barabara kwa watoto pindi waendapo shuleni.

Akisoma risala kwa mgeni rasmi mtendaji wa kata ya Ludete Aloyce Kamuli ameeleza kuwa pamoja na zoezi la kuendelea kujenga shule ya msingi ya Bwawani lakini bado wanachangamoto kubwa zaidi ya kukosekana shule ya sekondari katika kata hiyo hali ambayo imekuwa ikisababisha wanafunzi waliopo katani hapo kutembea umbali wa kilomita nyingi kufata elimu.

Akikabidhi msaada huo msemaji wa kampuni ya muya investment  kanda ya ziwa Rashid Hasan amefafanua kuwa lengo la kutoa mabati hayo ni  kuunga jitihada za  Raisi John Magufuli  za kuinua elimu nchini na kupambana na changamoto ambazo zimekuwa zikitokea mara kwa mara katika shule zilizopo nchini hapa.



Wakati huo huo meneja wa kampuni ya uchimbaji wa dhahabu ya ANDLU GOLDEN AND PATINZI Kurwa Sagwea  amekabidhi sh milioni 2 kwa ajili ya madawati katika shule ya msingi Subola kata ya kaseme  huku mkuu wa shule hiyo Steven Kibiliti akielezea kuwa  bado wanakabiliwa na  changamoto kubwa ya  upungufu wa madarasa shuleni hapo.


Akipokea misaada hiyo mkuu wa wilaya ya Geita Hermani Kapufi amepongeza makapuni hayo na kusema kwamba kwa kutoa msaada wao kwa moyo wanajiwekea hadhina mbinguni na kuwataka wengine kuiga mifano ya kuchangia maendeleo yao kwenye maeneo wanayoishi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here