Joh Makini ndiye aliyemfundisha Nick wa Pili kusoma na kuandika - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Thursday 6 October 2016

Joh Makini ndiye aliyemfundisha Nick wa Pili kusoma na kuandika

   13658704_1078612238893251_888944839_n
Nick wa Pili alikuwa mmoja wa wale watoto waliojua kusoma na kuandika (walau wa uchache) kwa kufundishwa tu nyumbani kabla ya kuanza shule rasmi.
Na ni kaka yake, Joh Makini ndiye alikuwa mwalimu wake wa kwanza.

“Joh Makini kwanza ndiye aliyenifundisha kusoma na kuandika kabla ya kuanza darasa la kwanza,” Nick alimwambia Prince Ramalove wa Kings FM.
Pamoja na kukiri kuwa kaka yake ni kichwa, haoni kama angependa kuja kuwa mwalimu.
“Sijui kama hicho kilikuwa ndani yake, lakini naona ni mtu mwenye akili sana, sijui nitamweka wapi lakini kama asingekuwa msanii angekuwa anafanya kitu kingine tu,” alieleza.

Nick wa Pili ni msomi wa shahada ya uzamili kwa sasa

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here