Mkurugenzi wa sensa na takwimu za jamii, Ephrahim Kwesigabo, amesema
mfumuko wa bei wa taifa wa Septemba mwaka huu umepungua mpaka kufikia asilimia
4.5 kutoka 4.9 ilivyokuwa Agosti.
Mkurugenzi
huyo amesema bidhaa za chakula zilizopungua bei ni samaki, dagaa,na viazi
vitamu.
“Uwezo wa shilingi 100 ya Tanzania
katika kununua bidhaa na huduma umefikia shilingi 97.04 kwa Septemba mwaka huu
kutoka Disemba 2015,ikilinganishwa na shilingi 96.83 iliyokuwa Agosti 2016”,
alisema Kwesigabo.
Aidha alisema kwa upande wa bidhaa
zisizo za chakula zilizopungua ni pamoja na gesi,petroli na dizeli.
BY: EMMY MWAIPOPO
No comments:
Post a Comment