Nay wa Mitego amedai kuwa kinachoendelea kati ya Barakah The Prince na
Stan Bakora, kinaweza kuwa kitu cha kutengeneza.
Akiongea
na mtangazaji wa Kings FM, Prince Ramalove, rapper huyo amewaita wawili hao
wote watoto na kwamba umri wao unawaruhusu kufanya wwanachokifanya.
“Siwezi kusimama upande wowote, hao
ni watoto, wote ni wadogo mimi ni wadogo zangu,” alisema.
“So inapofika time wanagombana
wataelewana tu. Hatuwezi kujua labda ni kiki, haiwezi kuwa beef kiasi hicho,
inawezekana labda kiki, watu mkachukulia serious kumbe wamekaa wametengeneza,”
ameongeza Nay.
Barakah ameonekana kuchukizwa na
parody aliyofanya Stan ya wimbo wake Nisamehe ambapo amejipaka masizi usoni
kuwa mweusi kama muimbaji huyo.
Stan amejipatia umaarufu kwa
kuigiza sauti ya Nay wa Mitego.
No comments:
Post a Comment