Wakazi wa Magomeni kota wilaya ya Kinondoni jijini Dar es Salaam,
wamefanya ibada maalum kwaajili ya kumuombea Rais Dkt John Magufuli ili aweze
kutekeleza azma yake kukamilisha ujenzi wa nyumba zao.
Akizungumza
katika ibada hiyo, mkuu wa wilaya ya Kinondoni, Ally Hapi, aliwapongeza wakazi
hao kwa hatua hiyo na kuwaahidi ushirikiano wake, akiwa msaidizi wa Rais
Magufuli wilayani humo.
“Tutapambana kuhakikisha kwamba
yale aliyoyaagiza mheshimiwa rais na yale anayokusudia kuyafanya,sisi kama
wasaidizi wake tunafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha kwamba tunayasimamia
na yanatekelezwa,” alisema.
Moambezi hayo yalijumuisha viongozi
wa dini mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali.
BY: EMMY MWAIPOPO
No comments:
Post a Comment