Mwanamke Amuuza Mwanawe wa Siku Tatu Siku ya Mwaka Mpya - OREST NGOWI

Breaking

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Post Top Ad

Responsive Ads Here

Friday 12 January 2018

Mwanamke Amuuza Mwanawe wa Siku Tatu Siku ya Mwaka Mpya


ITUI, KENYA: Mwanamke aliyejulikana kama Sarahi Kwamboka amepandishwa kizimbani kujibu tuhuma za kumuuza mwanae wa siku 3 siku ya mwaka mpya kwa dau la Shilingi 10,000 za Kenya.

Mtuhumiwa huyo ambaye ni Mama wa Watoto 3 alipandishwa kizimbani pamoja na anayedaiwa kumnunua mtoto huyo, Bi. Bernadette Musanya.
-
Korti ilielezwa kuwa Mtuhumiwa huyo wa kwanza alijifungua mtoto wa kike aitwaye Fridah Mutheu katika kituo cha afya cha Kanyangi siku ya Desemba 29, 2017 huko Kitui na siku 3 baadaye yaani siku ya mwaka mpya ndipo alimuuza kwa Bi. Musanya.
-
Wawili hao walikubali mashtaka ambapo mama huyo alidai amefanya hayo kutokana na umasikini unaomkabili na aliona atashindwa kumlea mtoto huyo pamoja na watoto wake wengine wawili.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Responsive Ads Here